Agosti tisa mewadia, sote Kwa hamu metarajia
Asifiwe yesu kenya kwanza, wanaazimio hallelujaa
Tumsifu yesu timu wajakoya, asifiwe kristo wanaprofesa
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe
Upendo umoja na amani, ndio tunu za kikristo
Wakristo tupendane nawasihi, Kwa maneno na vitendo
Kwa wengine vielelezo tuweni, alivyotufundisha yesu kristo
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe
Haki huinua taifa, ndivyo asemavyo ziraili
Amani na haki hazitadumishwa, tu Kwa ombi na usemi
Eti chama Fulani kikitawala, basi ndipo itaenea amani
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe
Ni jukumu letu wakristo, kujitofautisha na wengine
Wadada Kwa wandugu, jamani amani tuitende
Tuzidi kuwa mwanga, Nuru ya amani tuiangaze
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe
Ole ni wa taifa, Kwa sababu ya mambo ya kukosesha
Maana hayana budi, kuja mambo ya kukosesha
Lakini ole wake mtu yule, aliletaye jambo LA kukosesha
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe
Ninakusihi ewe ndugu, Dua kuipiga tuzidi
Amani ya mwenyezi Mungu, itawale yetu nchi
Amani, umoja na undugu, Kwa matendo tuiendeleze nasi
Amani ni ombi langu, sote tuidumishe.
~ Faith Nelima