Print this page
Wednesday, 29 June 2022 12:57

Tuenezeni Amani Featured

Written by Faith Weru
Rate this item
(1 Vote)

Watu wa nyumba "muriega" na wakamba "mwasyata"?

Wenzangu wa kakamega, ndugu zangu wataita

Wazee pia wachanga, hatuyataki matata

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

Kwa wakale "chamgei" na waluhya mm "vulai"?

Ndugu zangu wamasaai, mko "sopa" natumai

Nimekuja kuwarai, tusiwe na vurumai

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

Ni ujumbe ninaweka, upate Wakenya wengi

Je mwajua ni baraka, kuwa makabila mengi

Hili sitilie shaka, baraka hizi ni nyingi

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

Kabila sio, lisije kututawanya

Turkana na waluo, sisi wote ni wakenya

Sitaki kuwe kilio, cha lugha kutugawanya

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

Viongozi tuchague, waongoze nchi yetu chaguo

Mwenzio simchukie, tuwapende wenzetu

Vita tusizianzie, umoja ni nguvu yetu

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

Baada ya uchaguzi taendelea kuishi

Nawaambia kwa wazi, kenya kamwe haiishi

Tuuwache ubaguzi, na kwa upendo tuishi

Kwa umoja na upendo tuenezeni amani

Kwani kuna haja gani? Ndugu yako kuumiza

Na utafaidi na nini, mwenzako kimcharaza

Tukiikana amani, twajitia kwa gereza

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani.

Si lazima mtu wetu, ama pia mtu wenu

Sisi sote kenya yetu, si yangu wala si yenu

Hakuna huyu ni wetu, jirani yako ni wenu

Kwa umoja na upendo tuenezeni Amani

Ee Mungu nguvu yetu, dumisha upendo wetu

Na hii amani yetu, iwe hifadhi ya kwetu

Tutunze kilichochetu, migogoro siwe yetu.

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

~ Faith weru

   Almaarufu mchele wa chenga

Watu wa nyumba "muriega" na wakamba "mwasyata"?

Wenzangu wa kakamega, ndugu zangu wataita

Wazee pia wachanga, hatuyataki matata

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Kwa wakale "chamgei" na waluhya mm "vulai"?

Ndugu zangu wamasaai, mko "sopa" natumai

Nimekuja kuwarai, tusiwe na vurumai

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Ni ujumbe ninaweka, upate wakenya wengi

Je mwajua ni baraka, kuwa makabila mengi

Hili sitilie shaka, baraka hizi ni nyingi

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Kabila sio, lisije kututawanya

Turkana na waluo, sisi wote ni wakenya

Sitaki kuwe kilio, cha lugha kutugawanya

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Viongozi tuchague, waongoze nchi yetu chaguo

Mwenzio simchukie, tuwapende wenzetu

Vita tusizianzie, umoja ni nguvu yetu

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Baada ya uchaguzi taendelea kuishi

Nawaambia kwa wazi, kenya kamwe haiishi

Tuuwache ubaguzi, na kwa upendo tuishi

Kwa umoja na upendo tuenezeni amani

 

 

Eneza Amani

Kwani kuna haja gani? Ndugu yako kuumiza

Na utafaidi na nini, mwenzako kimcharaza

Tukiikana amani, twajitia kwa gereza

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani.

 

Si lazima mtu wetu, ama pia mtu wenu

Sisi sote kenya yetu, si yangu wala si yenu

Hakuna huyu ni wetu, jirani yako ni wenu

Kwa umoja na upendo tuenezeni Amani

 

Ee Mungu nguvu yetu, dumisha upendo wetu

Na hii amani yetu, iwe hifadhi ya kwetu

Tutunze kilichochetu, migogoro siwe yetu.

Kwa umoja na upendo, tuenezeni amani

 

Faith weru

Almaarufu mchele wa chenga

Read 502 times